1 Rum 12:16 BWANA, moyo wangu hauna kiburi,
Wala macho yangu hayainuki.
Wala sijishughulishi na mambo makuu,
Wala mambo yanayozidi nguvu zangu.
2 Mt 18:3 Hakika nimeituliza nafsi yangu,
Na kuinyamazisha.
Kama mtoto aliyeachishwa kunyonya
Kifuani mwa mama yake;
Roho yangu ni kama mtoto,
Aliyeachishwa kunyonya.
3Ee Israeli, umtarajie BWANA,
Tangu leo na hata milele.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.