1Haleluya.
Nitamshukuru BWANA kwa moyo wangu wote,
Barazani pa wanyofu wa moyo na katika mkutano.
2 Ayu 38:1 Matendo ya BWANA ni makuu,
Yafikiriwa sana na wapendezwao nayo.
3Kazi yake imejaa heshima na adhama,
Na haki yake yadumu milele.
4Amefanya ukumbusho wa matendo yake ya ajabu;
BWANA ni mwenye fadhili na rehema.
5Amewapa wamchao chakula;
Atalikumbuka agano lake milele.
6Amewajulisha watu wake uwezo wa matendo yake,
Kwa kuwapa urithi wa mataifa.
7 Zab 19:7 Matendo ya mikono yake ni kweli na hukumu,
Maagizo yake yote ni amini,
8 Ufu 15:3 Yamethibitika milele na milele,
Yamefanywa kwa uaminifu na haki.
9 Ufu 15:3 Amewapelekea watu wake ukombozi,
Ameamuru agano lake liwe la milele,
Jina lake ni takatifu na la kuogopwa.
10 Kum 4:6; Ayu 28:28; Mit 1:7; 9:10; Mhu 12:3 Kumcha BWANA ndio mwanzo wa hekima,
Wote wafanyao hayo wana ufahamu mzuri,
Sifa zake zadumu milele.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.