Isaya 60 - Swahili, Common Language Bible with DCs

Yerusalemu mpya

1Inuka ee Siyoni uangaze;

maana mwanga unachomoza kwa ajili yako,

utukufu wa Mwenyezi-Mungu unakuangaza.

2Tazama, giza litaifunika dunia,

giza nene litayafunika mataifa;

lakini wewe, Mwenyezi-Mungu atakuangazia,

utukufu wake utaonekana kwako.

3Mataifa yataujia mwanga wako,

wafalme waujia mwanga wa pambazuko lako.

4Inua macho utazame pande zote;

wote wanakusanyika waje kwako.

Wanao wa kiume watafika toka mbali,

wanao wa kike watabebwa mikononi.

5Utaona na uso wako utangara,

moyo wako utasisimka na kushangilia.

Maana utajiri wa bahari utakutiririkia,

mali za mataifa zitaletwa kwako.

6Makundi ya ngamia yataifunika nchi yako,

naam, ndama wa ngamia kutoka Midiani na Efa;

wote kutoka Sheba watakuja.

Watakuletea dhahabu na ubani,

wakitangaza sifa za Mwenyezi-Mungu.

7Makundi ya kondoo wa Kedari yatakusanywa kwako,

utaweza kuwatumia kondoo madume wa Nebayothi kuwa kafara;

utawatoa kuwa tambiko inayokubalika madhabahuni pa Mungu,

naye ataitukuza nyumba yake tukufu.

8Nani hao wanaopepea kama mawingu,

kama njiwa wanaoruka kwenda viotani mwao?

9Ni meli zitokazo nchi za mbali,

zikitanguliwa na meli za Tarshishi.

Zinawaleta watoto wako,

pamoja na fedha na dhahabu yao,

kwa sifa ya Mwenyezi-Mungu, Mungu wako,

kwa sifa ya Mungu, Mtukufu wa Israeli,

maana amewafanya mtukuke.

10Mwenyezi-Mungu asema:

“Wageni watazijenga upya kuta zako,

wafalme wao watakutumikia.

Maana kwa hasira yangu nilikupiga,

lakini kwa fadhili yangu nimekuhurumia.

11

19 60:19 Taz Ufu 21:23, 22:5 “Hutahitaji tena jua kukuangazia mchana,

wala mwezi kukumulikia usiku;

maana mimi Mwenyezi-Mungu ni mwanga wako milele;

mimi Mungu wako nitakuwa fahari yako.

20Mwanga wako mchana hautatua kama jua,

wala mwangaza wako usiku kufifia kama mbalamwezi;

maana Mwenyezi-Mungu ni mwanga wako milele,

nazo siku zako za kuomboleza zitakoma.

21Watu wako wote watakuwa waadilifu,

nao wataimiliki nchi milele.

Hao ni chipukizi nililopanda mimi,

kazi ya mikono yangu kwa ajili ya utukufu wangu.

22Aliye mdogo kati yenu atakuwa ukoo,

aliye mdogo kuliko wote atakuwa taifa kubwa.

Mimi ndimi Mwenyezi-Mungu;

wakati ufikapo nitayatekeleza hayo haraka.”

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help