Zaburi 121 - Swahili, Common Language Bible with DCs

Mungu kinga yetu(Wimbo wa Kwenda Juu, wa Daudi)

1Natazama juu milimani;

msaada wangu utatoka wapi?

2Msaada wangu watoka kwa Mwenyezi-Mungu,

aliyeumba mbingu na dunia.

3Hatakuacha uanguke;

mlinzi wako hasinzii.

4Kweli mlinzi wa Israeli

hasinzii wala halali.

5Mwenyezi-Mungu ni mlinzi wako;

yuko upande wako wa kulia kukukinga.

6Mchana jua halitakuumiza,

wala mwezi wakati wa usiku.

7Mwenyezi-Mungu atakukinga na baya lolote;

atayalinda salama maisha yako.

8Mwenyezi-Mungu atakulinda katika shughuli zako zote

tangu sasa na hata milele.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help