Zaburi 128 - Swahili, Common Language Bible with DCs

Tuzo kwa jamaa imchayo Mungu(Wimbo wa Kwenda Juu)

1Heri wote wamchao Mwenyezi-Mungu,

wanaoishi kufuatana na amri zake.

2Utapata matunda ya jasho lako,

utafurahi na kupata fanaka.

3Mkeo atakuwa kama mzabibu wa matunda mengi nyumbani mwako;

watoto wako kama chipukizi za mzeituni kuzunguka meza yako.

4Naam, ndivyo atakavyobarikiwa

mtu amchaye Mwenyezi-Mungu.

5Mwenyezi-Mungu akubariki kutoka Siyoni!

Uione fanaka ya Yerusalemu, siku zote za maisha yako.

6Uishi na hata uwaone wajukuu zako!

Amani iwe na Israeli!

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help