Zaburi 96 - Swahili, Common Language Bible with DCs

Mungu mfalme na hakimu(1Nya 16:23-33)

1Mwimbieni Mwenyezi-Mungu wimbo mpya!

Mwimbieni Mwenyezi-Mungu, ulimwengu wote!

2Mwimbieni Mwenyezi-Mungu na kulisifu jina lake.

Tangazeni kila siku matendo yake ya wokovu.

3Yatangazieni mataifa utukufu wake,

waambieni watu wote matendo yake ya ajabu.

4Maana Mwenyezi-Mungu ni mkuu, anasifika sana;

anastahili kuheshimiwa kuliko miungu yote.

5Miungu ya mataifa mengine si kitu;

lakini Mwenyezi-Mungu aliziumba mbingu.

6Utukufu na fahari vyamzunguka;

nguvu na uzuri vyalijaza hekalu lake.

7

tetemekeni mbele yake ee dunia yote!

10Yaambieni mataifa: “Mwenyezi-Mungu anatawala!

Ameuweka ulimwengu imara, hautatikisika.

Atawahukumu watu kwa haki!”

11Furahini enyi mbingu na dunia!

Bahari na ivume pamoja na vyote vilivyomo!

12Furahini enyi mashamba na vyote vilivyomo!

Ndipo miti yote misituni itaimba kwa furaha,

13mbele ya Mwenyezi-Mungu anayekuja;

naam, anayekuja kuihukumu dunia.

Ataihukumu dunia kwa haki,

na mataifa kwa uaminifu wake.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help