1Ni jambo zuri na la kupendeza sana
ndugu kuishi pamoja kwa umoja.
2Ni kama mafuta mazuri yatiririkayo kichwani,
mpaka kwenye ndevu zake Aroni,
mpaka upindoni mwa vazi lake shingoni.
3Ni kama umande wa mlima Hermoni,
uangukao juu ya vilima vya Siyoni!
Huko Mwenyezi-Mungu ameahidi kuwabariki watu wake,
kuwapa uhai usio na mwisho.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.