1
22“Enyi wajinga! Mpaka lini mtapenda kuwa wajinga?
Mpaka lini wenye dharau watafurahia dharau zao,
na wapumbavu kuchukia maarifa?
23Sikilizeni maonyo yangu;
nitawamiminia mawazo yangu,
nitawajulisha maneno yangu.
24Kwa kuwa nimewaita mkakataa kusikiliza,
nimewapungia mkono mje mkakataa,
25mkapuuza mashauri yangu yote,
wala hamkuyajali maonyo yangu,
26nami pia nitayachekelea maafa yenu,
nitawadhihaki mnapokumbwa na hofu,
27hofu itakapowakumba kama tufani,
maafa yenu yatakapowavamia kama kimbunga,
wakati udhia na dhiki vitakapowapata.
28Hapo ndipo mtakaponiita lakini sitaitika;
mtanitafuta kwa bidii lakini hamtanipata.
29Kwa kuwa mliyachukia maarifa,
wala hamkuchagua kumcha Mwenyezi-Mungu;
30maadamu mlikataa shauri langu,
mkayapuuza maonyo yangu yote;
31basi, mtakula matunda ya mienendo yenu,
mtavimbiwa kwa hila zenu wenyewe.
32Maana wajinga hujiua kwa ukaidi wao,
wapumbavu hujiangamiza kwa kujiamini kwao.
33Lakini kila anisikilizaye atakaa salama,
atatulia bila kuogopa mabaya.”
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.