1Ee Mwenyezi-Mungu, mkumbuke Daudi,
kumbuka taabu zote alizopata.
2Ukumbuke ahadi aliyokupa, ee Mwenyezi-Mungu,
kiapo alichokuapia, ewe Mwenye Nguvu wa Yakobo:
3“Sitaingia ndani ya nyumba yangu,
wala kulala kitandani mwangu;
4sitakubali kulala usingizi,
wala kusinzia;
5mpaka nikupatie wewe Mwenyezi-Mungu mahali pa kukaa,
makao yako, ewe Mwenye Nguvu wa Yakobo!”
6Huko Efratha tulisikia habari za sanduku la agano,
tukalikuta katika mashamba ya Yearimu.
7“Haya! Twende nyumbani kwa Mungu,
tuabudu mbele ya kiti chake cha enzi!”
8Inuka ee Mwenyezi-Mungu, nenda kwenye maskani yako;
inuka pamoja na sanduku la agano la uwezo wako!
9Makuhani wako wawe waadilifu daima;
na waaminifu wako wapige vigelegele vya furaha!
10Kwa ajili ya Daudi, mtumishi wako,
usimkatae huyo mfalme uliyemweka wakfu.
11
waaminifu wake watapiga vigelegele vya furaha.
17Humo nitamchipusha mfalme shujaa wa ukoo wa Daudi:
Kama taa iwakayo nitamtegemeza mfalme niliyemteua.
18Maadui zake nitawavika aibu;
lakini yeye nitamvika fahari ya kifalme.”
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.