Zaburi 120 - Swahili, Common Language Bible with DCs

Kuomba msaada(Wimbo wa Kwenda Juu)

1Katika taabu yangu nilimwita Mwenyezi-Mungu,

naye akanijibu.

2Uniokoe ee Mwenyezi-Mungu,

na watu wadanganyifu na waongo.

3Enyi watu wadanganyifu, mtapewa kitu gani?

Mtaadhibiwa namna gani?

4Kwa mishale mikali ya askari,

kwa makaa ya moto mkali!

5Ole wangu kwamba naishi kama mgeni huko Mesheki;

naishi kama mgeni katika mahema ya Kedari.

6Nimeishi muda mrefu mno

kati ya watu wanaochukia amani!

7Wakati ninaposema nataka amani,

wao wanataka tu vita.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help