Zaburi 122 - Swahili, Common Language Bible with DCs

Sifa za Yerusalemu(Wimbo wa Kwenda Juu, wa Daudi)

1Nilifurahi waliponiambia:

“Twende nyumbani kwa Mwenyezi-Mungu.”

2Sasa tuko tumesimama,

kwenye malango yako, ee Yerusalemu!

3Yerusalemu, mji uliojengwa,

ili jumuiya ikutane humo.

4Humo ndimo makabila yanamofika,

naam, makabila ya Israeli,

kumshukuru Mwenyezi-Mungu kama alivyoagiza.

5Humo mmewekwa mahakama ya hukumu ya haki,

mahakama ya ukoo wa kifalme wa Daudi.

6Uombeeni Yerusalemu amani:

“Wote wakupendao na wafanikiwe!

7Ndani ya kuta zako kuwe na amani,

majumbani mwako kuweko usalama!”

8Kwa ajili ya jamaa na ndugu zangu,

ee Yerusalemu, nakutakia amani!

9Kwa ajili ya nyumba ya Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu,

ninakuombea upate fanaka!

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help