Zaburi 29 - Swahili, Common Language Bible with DCs

Sauti ya Mungu katika dhoruba(Zaburi ya Daudi)

1

3Sauti ya Mwenyezi-Mungu yasikika juu ya maji;

Mungu mtukufu angurumisha radi,

sauti ya Mwenyezi-Mungu yasikika juu ya bahari!

4Sauti ya Mwenyezi-Mungu ina nguvu,

sauti ya Mwenyezi-Mungu imejaa fahari.

5Sauti ya Mwenyezi-Mungu huvunja mierezi;

Mwenyezi-Mungu avunja mierezi ya Lebanoni.

6Huirusha milima ya Lebanoni kama ndama,

milima ya Sirioni kama mwananyati.

7Sauti ya Mwenyezi-Mungu hutoa miali ya moto.

8Sauti ya Mwenyezi-Mungu hutetemesha jangwa,

Mwenyezi-Mungu hutetemesha jangwa la Kadeshi.

9Sauti ya Mwenyezi-Mungu huitikisa mivule,

hukwanyua majani ya miti msituni,

na hekaluni mwake wote wasema:

“Utukufu kwa Mungu!”

10Mwenyezi-Mungu ameketi juu ya gharika;

Mwenyezi-Mungu ni mfalme atawalaye milele.

11Mwenyezi-Mungu na awape watu wake nguvu!

Mwenyezi-Mungu na awabariki watu wake kwa amani!

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help