Zaburi 142 - Swahili, Common Language Bible with DCs

Dua ya mtu aliyeachwa mpweke(Utenzi wa Daudi alipokuwa pangoni. Sala)

1Namlilia Mwenyezi-Mungu kwa sauti,

namsihi Mwenyezi-Mungu kwa sauti yangu.

2Namwekea malalamiko yangu,

namweleza taabu zangu.

3Ninapokaribia kukata tamaa kabisa,

yeye yupo, anajua mwenendo wangu.

Maadui wamenitegea mitego njiani mwangu.

4Nikiangalia upande wa kulia na kungojea,

naona hakuna mtu wa kunisaidia;

sina tena mahali pa kukimbilia,

hakuna mtu anayenijali.

5Nakulilia wewe, ee Mwenyezi-Mungu!

Wewe ni kimbilio langu la usalama;

wewe ni riziki yangu kuu katika nchi ya walio hai.

6Usikilize kilio changu, maana nimekuwa hoi;

uniokoe na watesi wangu, maana wamenizidi nguvu.

7Unitoe humu kifungoni,

ili nipate kukushukuru.

Watu waadilifu watajiunga nami

kwa sababu umenitendea mema mengi.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help