1Upende kuniokoa ee Mungu!
Ee Mwenyezi-Mungu, uje haraka kunisaidia.
2Wanaonuia kuniangamiza,
na waaibike na kufedheheka!
Hao wanaotamani niumie,
na warudi nyuma na kuaibika.
3Hao wanaonisimanga,
na wapumbazike kwa kushindwa kwao.
4Lakini wote wale wanaokutafuta,
wafurahi na kushangilia kwa sababu yako.
Wapendao wokovu wako,
waseme daima: “Mungu ni mkuu!”
5Nami niliye maskini na fukara,
unijie haraka, ee Mungu!
Ndiwe msaada wangu na mkombozi wangu;
ee Mwenyezi-Mungu, usikawie!
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.