Zaburi 138 - Swahili, Common Language Bible with DCs

Sala ya shukrani

1Nakushukuru, ee Mwenyezi-Mungu, kwa moyo wangu wote,

naimba sifa zako mbele ya miungu.

2Ninasujudu kuelekea hekalu lako takatifu;

nalisifu jina lako,

kwa sababu ya fadhili zako na uaminifu wako;

kwa sababu umeweka jina lako na neno lako

juu ya kila kitu.

3Nilipokulilia, wewe ulinijibu;

umeniongezea nguvu zangu.

4Wafalme wote duniani watakusifu, ee Mwenyezi-Mungu,

kwa sababu wameyasikia maneno yako.

5Wataimba sifa za matendo yako, ee Mwenyezi-Mungu,

kwa maana utukufu wako ni mkuu.

6Ingawa wewe ee Mwenyezi-Mungu, uko juu ya wote,

unawaangalia kwa wema walio wanyonge;

nao wenye kiburi huwaona kutoka mbali.

7Hata nikikumbana na taabu, wewe wanilinda;

waunyosha mkono wako dhidi ya hasira ya maadui zangu wakali;

kwa nguvu yako kuu wanisalimisha.

8Ee Mwenyezi-Mungu, utatimiza yote uliyoniahidi.

Fadhili zako, ee Mwenyezi-Mungu, zadumu milele.

Usisahau kazi ya mkono wako mwenyewe.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help