Zaburi 101 - Swahili, Common Language Bible with DCs

Mwongozo mzuri wa mfalme(Zaburi ya Daudi)

1Utenzi wangu kuhusu uaminifu na haki;

ninauimba kwa heshima yako, ee Mwenyezi-Mungu.

2Nitazingatia mwenendo usio na hatia.

Je, utakuja kwangu lini?

Nitaishi kwa unyofu nyumbani kwangu;

3sitavumilia kamwe upuuzi.

Nayachukia matendo ya watu wapotovu,

mambo yao hayataambatana nami.

4Upotovu wowote ule uwe mbali nami;

sitahusika kabisa na uovu.

5Anayemsengenya jirani nitamfutilia mbali;

sitamvumilia mwenye majivuno na kiburi.

6Nitawaangalia kwa wema watu walio waaminifu,

wapate kuishi pamoja nami.

Watu wanyofu ndio watakaonitumikia.

7Mwongo yeyote hatakaa nyumbani mwangu;

hakuna msema uongo atakayekaa kwangu.

8Siku kwa siku nitawaangamiza waovu wote nchini;

nitawaangamiza wabaya wote mjini mwa Mwenyezi-Mungu.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help