Zaburi 53 - Swahili, Common Language Bible with DCs

Mtu asiyemcha Mungu(taz Zaburi ya 14)(Kwa Mwimbishaji: Mtindo wa Mahalathi. Utenzi wa Daudi)

1 Rom 3:10-12 Wapumbavu hujisemea moyoni:

“Hakuna Mungu!”

Wote wamepotoka kabisa,

wametenda mambo ya kuchukiza;

hakuna hata mmoja atendaye jema.

2Mungu anawaangalia wanadamu kutoka mbinguni,

aone kama kuna yeyote mwenye busara,

kama kuna yeyote anayemtafuta Mungu.

3Lakini wote wamekosa,

wote wamepotoka pamoja,

hakuna atendaye mema,

hakuna hata mmoja.

4“Je, hao watendao maovu hawana akili?

Wanawatafuna watu wangu kama mikate;

wala hawanijali mimi Mungu!”

5Hapo watashikwa na hofu kubwa,

hofu ambayo hawajapata kuiona;

maana Mungu ataitawanya mifupa ya adui,

hao wataaibika maana Mungu amewakataa.

6Laiti ukombozi wa Israeli ungefika kutoka Siyoni!

Mungu atakaporekebisha hali ya watu wake,

wazawa wa Yakobo watashangilia;

Waisraeli watafurahi.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help