1Karibieni mkasikilize enyi mataifa,
tegeni sikio enyi watu.
Sikiliza ee dunia na vyote vilivyomo,
ulimwengu na vyote vitokavyo humo!
2Mwenyezi-Mungu ameyakasirikia mataifa yote,
ameghadhabika dhidi ya majeshi yao yote.
Ameyapangia mwisho wao,
ameyatoa yaangamizwe.
3Maiti zao zitatupwa nje;
harufu ya maiti zao itasambaa;
milima itatiririka damu yao.
4 yataitana humo;
kwao usiku utakuwa mwanga,
na humo watapata mahali pa kupumzikia.
15Humo bundi watataga mayai na kuyaatamia,
wataangua vifaranga na kuviweka kivulini mwao.
Humo vipanga watakutania,
kila mmoja na mwenzake.
16Someni katika kitabu cha Mwenyezi-Mungu:
“Hakuna hata kiumbe kimoja kitakachokosekana,
kila kimoja kitakuwako na mwenzake.”
Maana Mwenyezi-Mungu mwenyewe ametamka hivyo,
roho yake itawakusanya hao wote.
17Mwenyezi-Mungu amepanga sehemu ya kila mmoja wao,
ametumia kamba kuwapimia nchi hiyo;
wataimiliki milele na milele,
wataishi humo kizazi hata kizazi.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.