Isaya 12 - Swahili, Common Language Bible with DCs

Wimbo wa shukrani

1Siku hiyo mtasema:

“Nakushukuru, ee Mwenyezi-Mungu,

maana ingawa ulinikasirikia,

hasira yako imetulia,

nawe umenifariji.

2 12:2 Taz Kut 15:2; Zab 118:14 Mungu ndiye mwenye kuniokoa,

nitamtegemea yeye, wala sitaogopa;

Mwenyezi-Mungu hunijalia nguvu;

yeye mwenyewe ndiye aniokoaye.”

3Mtachota maji kwa furaha

kutoka visima vya wokovu.

4Siku hiyo mtasema:

“Mshukuruni Mwenyezi-Mungu

mwombeni kwa jina lake.

Yajulisheni mataifa matendo yake,

tangazeni kuwa jina lake limetukuka.

5Mwimbieni Mwenyezi-Mungu sifa

kwa kuwa ametenda mambo makuu;

haya na yajulikane duniani kote.

6Pazeni sauti na kuimba kwa furaha,

enyi wakazi wa Siyoni,

maana aliye mkuu miongoni mwenu

ndiye Mungu, Mtakatifu wa Israeli.”

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help