Hosea 6 - Kiswahili Study Bible

Toba isiyo ya kweli

1“‘Twendeni, tukamrudie Mwenyezi-Mungu!

Yeye mwenyewe ameturarua,

lakini yeye mwenyewe atatuponya.

Yeye mwenyewe ametujeruhi,

lakini yeye mwenyewe atatibu majeraha yetu.

2Baada ya siku mbili, atatupa uhai tena,

naam, siku ya tatu atatufufua

ili tuweze kuishi pamoja naye.

3Basi tumtambue,

tujitahidi kumjua Mwenyezi-Mungu.

Kuja kwake ni hakika kama alfajiri,

yeye atatujia kama manyunyu,

kama mvua za masika ziinyweshayo ardhi.’”

4Lakini Mwenyezi-Mungu asema hivi:

“Nitakutendea nini ee Efraimu?

Nikufanyie nini ee Yuda?

Upendo wenu kwangu ni kama ukungu wa asubuhi,

kama umande unaotoweka upesi.

5Ndiyo maana nimewavamia kwa njia ya manabii,

nimewaangamiza kwa maneno yangu,

hukumu yangu huchomoza kama pambazuko.

6Maana ninachotaka kwenu ni upendo na si tambiko,

Kumjua Mungu na si kutoa sadaka za kuteketezwa.

Uhalifu umeenea kote nchini

7“Lakini mlilivunja agano langu

kama mlivyofanya mjini Adamu;

huko walinikosea uaminifu.

8Gileadi ni mji wa waovu,

umetapakaa damu.

9Kama wanyang'anyi wamwoteavyo mtu njiani,

ndivyo na makuhani walivyojikusanya na kuvizia.

Wanaua watu njiani kuelekea Shekemu,

naam, wanatenda uovu kupindukia.

10Nimeona jambo la kuchukiza sana

miongoni mwa Waisraeli:

watu wa Efraimu wanakimbilia miungu mingine

naam, Waisraeli wamejitia unajisi.

11Nawe Yuda hali kadhalika,

nimekupangia wakati utakapovuna adhabu.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help