Zaburi 15 - Kiswahili Study Bible

Rafiki ya Mungu(Zaburi ya Daudi)

1Nani ee Mwenyezi-Mungu atakayekaa hemani mwako?

Nani atakayeishi juu ya mlima wako mtakatifu?

2Ni mtu aishiye bila lawama,

atendaye daima yaliyo mema,

asemaye ukweli kutoka moyoni;

3ni mtu asiyesengenya watu,

asiyemtendea uovu rafiki yake,

wala kumfitini jirani yake;

4ni mtu anayewadharau wafisadi,

lakini huwaheshimu wamchao Mwenyezi-Mungu;

ni mtu asiyegeuza kiapo chake hata kikimtia hasara;

5asiyekopesha fedha yake kwa riba,

wala kupokea rushwa kumdhulumu asiye na hatia.

Mtu atendaye hayo,

kamwe hatatikisika.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help