Zaburi 141 - Kiswahili Study Bible

Hatari za tamaa mbaya(Zaburi ya Daudi)

1Nakuita, ee Mwenyezi-Mungu,

uje haraka kunisaidia!

Uisikilize sauti yangu wakati ninapokuita!

2Sala yangu uipokee kama ubani;

niinuapo mikono yangu kwako unikubali kama tambiko ya jioni.

3Ee Mwenyezi-Mungu ukilinde kinywa changu,

uweke ulinzi mlangoni mwa mdomo wangu.

4Unikinge nisielekee kufanya mabaya,

nisijishughulishe na matendo maovu;

nisijiunge na watu watendao mabaya,

wala nisishiriki kamwe karamu zao.

5Afadhali mtu mwema anipige kunionya;

lakini sikubali kamwe kusifiwa na wabaya,

maana nasali daima dhidi ya maovu yao.

6Wakuu wao watakapopondwa miambani,

ndipo watatambua maneno yangu yalikuwa sawa.

7Mifupa yao itatawanywa mdomoni pa Kuzimu

kama kuni zilizopasuliwa vipandevipande!

8Bali mimi nakutegemea, ee Mwenyezi-Mungu, Mungu wangu;

ninakimbilia usalama kwako, usiniache hatarini.

9Unikinge na mitego waliyonitegea,

uniepushe na matanzi ya hao watu waovu.

10Waovu wanaswe katika mitego yao wenyewe,

wakati mimi najiendea zangu salama.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help