Zaburi 100 - Kiswahili Study Bible

Wimbo wa sifa(Zaburi ya shukrani)

1Mshangilieni Mwenyezi-Mungu, enyi nchi zote!

2Mwabuduni Mwenyezi-Mungu kwa furaha,

nendeni kwake mkiimba kwa shangwe!

3Jueni kwamba Mwenyezi-Mungu ni Mungu.

Yeye ndiye aliyetuumba, nasi ni mali yake;

sisi ni watu wake, ni kondoo wa malisho yake.

4Pitieni milango ya hekalu lake kwa shukrani,

ingieni katika nyua zake kwa sifa.

Mshukuruni na kulisifu jina lake.

5Mwenyezi-Mungu ni mwema;

fadhili zake zadumu milele,

na uaminifu wake katika vizazi vyote.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help