Zaburi 110 - Kiswahili Study Bible

Kutawazwa kwa mfalme mteule(Zaburi ya Daudi)

1Mwenyezi-Mungu amwambia bwana wangu:

“Keti upande wangu wa kulia,

hata niwaweke maadui zako chini ya miguu yako.”

2Mwenyezi-Mungu ataeneza enzi yako kutoka Siyoni;

utatawala juu ya maadui zako wote.

3Watu wako watakujia kwa hiari,

siku utakapokwenda kuwapiga maadui.

Juu ya milima mitakatifu watakujia vijana wako,

kama umande unaotokeza alfajiri mapema.

4Mwenyezi-Mungu amekuapia wala hatabadili nia yake:

“Wewe ni kuhani milele kwa utaratibu wa ukuhani wa Melkisedeki.”

5Bwana yuko upande wako wa kulia;

atawaponda wafalme atakapokasirika.

6Atayahukumu mataifa na kuwaua watu wengi;

atawaponda viongozi kila mahali duniani.

7Mfalme atakunywa maji ya kijito njiani;

naye atainua kichwa juu kwa ushindi.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help