Zaburi 2 - Kiswahili Study Bible

Mfalme mteule wa Mungu

1Kwa nini mataifa yanafanya ghasia?

Mbona watu wanafanya njama za bure?

2Wafalme wa dunia wanajitayarisha;

watawala wanashauriana pamoja,

dhidi ya Mwenyezi-Mungu na mteule wake.

3Wanasema: “Tujiondoe katika utawala wao;

tutupilie mbali minyororo yao!”

4Mwenyezi-Mungu atawalaye juu mbinguni,

anawacheka na kuwadhihaki.

5Kisha, anawakaripia kwa ghadhabu,

na kuwatisha kwa hasira, akisema:

6“Nimemtawaza mfalme niliyemteua,

anatawala Siyoni, mlima wangu mtakatifu!”

7

Mungu aliniambia:

‘Wewe ni mwanangu,

mimi leo nimekuwa baba yako.

8Niombe nami nitakupa mataifa yawe urithi wako,

na dunia nzima kuwa mali yako.

9Utawaponda kwa fimbo ya chuma;

utawavunja kama chungu cha mfinyanzi!’”

10Sasa enyi wafalme, tumieni busara;

sikilizeni onyo hili, enyi watawala wa dunia.

11Mtumikieni Mwenyezi-Mungu kwa uchaji;

12msujudieni na kutetemeka;

asije akakasirika, mkaangamia ghafla;

kwani hasira yake huwaka haraka.

Heri yao wote wanaokimbilia usalama kwake!

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help