Zaburi 93 - Kiswahili Study Bible

Mungu mfalme

1Mwenyezi-Mungu anatawala;

amejivika fahari kuu!

Mwenyezi-Mungu amevaa fahari na nguvu!

Ameuimarisha ulimwengu, nao hautatikisika kamwe.

2Kiti chako cha enzi ni imara tangu kale;

wewe umekuwapo kabla ya nyakati zote.

3Vilindi vimetoa sauti, ee Mwenyezi-Mungu;

naam, vimepaza sauti yake,

vilindi vyapaza tena mvumo wake.

4Mwenyezi-Mungu ana enzi kuu juu mbinguni,

ana nguvu kuliko mlio wa bahari,

ana nguvu kuliko mawimbi ya maji.

5Ee Mwenyezi-Mungu, maagizo yako ni thabiti;

nyumba yako ni takatifu milele na milele.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help