Zaburi 23 - Kiswahili Study Bible

Mungu mchungaji wangu(Zaburi ya Daudi)

1Mwenyezi-Mungu ni mchungaji wangu,

sitapungukiwa na kitu.

2Hunipumzisha kwenye malisho mabichi;

huniongoza kando ya maji matulivu,

3na kuirudishia nafsi yangu nguvu mpya.

Huniongoza katika njia sawa

kwa hisani yake.

4Nijapopita katika bonde la giza kuu la kifo,

sitaogopa hatari yoyote,

maana wewe ee Mwenyezi-Mungu u pamoja nami;

gongo lako na fimbo yako vyanilinda.

5Umeniandalia karamu mbele ya maadui zangu;

umenipaka mafuta kichwani pangu;

kikombe changu umekijaza mpaka kufurika.

6Kweli wema wako na fadhili zako zitakuwa pamoja nami,

siku zote za maisha yangu;

nami nitakaa nyumbani mwa Mwenyezi-Mungu milele.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help