Zaburi 124 - Kiswahili Study Bible

Mungu kinga yetu(Wimbo wa Kwenda Juu, wa Daudi)

1“Kama Mwenyezi-Mungu asingalikuwa upande wetu…”

Semeni nyote mlio katika Israeli:

2“Kama Mwenyezi-Mungu asingalikuwa upande wetu,

wakati ule tuliposhambuliwa na maadui,

3hakika tungalimezwa tukiwa hai,

wakati hasira zao zilipotuwakia.

4Tungalikumbwa na gharika,

tungalifunikwa na mto wa maji,

5mkondo wa maji ungalituchukua!”

6Atukuzwe Mwenyezi-Mungu,

ambaye hakutuacha makuchani mwao.

7Tumeponyoka kama ndege mtegoni;

mtego umeteguliwa, nasi tukaokoka.

8Msaada wetu watoka kwa Mwenyezi-Mungu,

aliyeumba mbingu na dunia.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help