1“Kama Mwenyezi-Mungu asingalikuwa upande wetu…”
Semeni nyote mlio katika Israeli:
2“Kama Mwenyezi-Mungu asingalikuwa upande wetu,
wakati ule tuliposhambuliwa na maadui,
3hakika tungalimezwa tukiwa hai,
wakati hasira zao zilipotuwakia.
4Tungalikumbwa na gharika,
tungalifunikwa na mto wa maji,
5mkondo wa maji ungalituchukua!”
6Atukuzwe Mwenyezi-Mungu,
ambaye hakutuacha makuchani mwao.
7Tumeponyoka kama ndege mtegoni;
mtego umeteguliwa, nasi tukaokoka.
8Msaada wetu watoka kwa Mwenyezi-Mungu,
aliyeumba mbingu na dunia.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.