Zaburi 4 - Kiswahili Study Bible

Kuomba msaada jioni(Kwa Mwimbishaji: na ala za nyuzi za muziki. Zaburi ya Daudi)

1Ee Mungu mtetezi wa haki yangu, unijibu niombapo.

Nilipokuwa katika shida, wewe ulinisaidia;

unionee huruma na kusikia sala yangu.

2Jamani, mtaniharibia jina langu mpaka lini?

Mpaka lini mtapenda upuuzi na kusema uongo?

3Jueni kuwa Mwenyezi-Mungu amejiteulia mwaminifu wake.

Mwenyezi-Mungu husikia kila ninapomwomba.

4Tetemekeni kwa hofu na msitende dhambi;

tafakarini vitandani mwenu na kunyamaza.

5Toeni tambiko zilizo sawa,

na kumtumainia Mwenyezi-Mungu.

6Wengi husema: “Laiti tungepata tena fanaka!

Utuangalie kwa wema, ee Mwenyezi-Mungu!”

7Lakini mimi umenijalia furaha kubwa moyoni,

kuliko ya hao walio na divai na ngano kwa wingi.

8Nalala na kupata usingizi kwa amani;

ee Mwenyezi-Mungu, wewe peke yako waniweka salama.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help