Zaburi 43 - Kiswahili Study Bible

Sala ya mkimbizi yaendelea(Zaburi ya 42 yaendelea)

1Onesha kuwa sina hatia ee Mungu;

utetee kisa changu dhidi ya watu wabaya;

uniokoe na watu waongo na waovu.

2Nakimbilia usalama kwako ee Mungu;

kwa nini umenitupilia mbali?

Yanini niende huko na huko nikiomboleza

kwa kudhulumiwa na adui yangu?

3Upeleke mwanga na ukweli wako viniongoze,

vinipeleke kwenye mlima wako mtakatifu,

kwenye makao yako.

4Hapo, ee Mungu, nitakwenda madhabahuni pako;

nitakuja kwako, ee Mungu, furaha yangu kuu.

Nitakusifu kwa zeze, ee Mungu, Mungu wangu.

5Mbona ninahuzunika hivyo moyoni?

Kwa nini nahangaika hivyo ndani mwangu?

Nitamtumainia Mungu,

nitamsifu tena

yeye aliye msaada wangu na Mungu wangu.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help