1Haleluya! Msifuni Mwenyezi-Mungu!
Mshukuruni Mwenyezi-Mungu kwa kuwa ni mwema;
kwa maana fadhili zake zadumu milele!
2Ni nani awezaye kutaja matendo ya Mwenyezi-Mungu?
Ni nani awezaye kumsifu kama anavyostahili?
3Heri wale wanaotekeleza haki,
wanaotenda daima mambo yaliyo sawa.
4Unikumbuke ee Mwenyezi-Mungu unapowafadhili watu wako;
unisaidie wakati unapowaokoa;
5ili niweze kuona fanaka ya wateule wako,
nipate kufurahia furaha ya taifa lako,
na kuona fahari pamoja na watu wako.
6Tumetenda dhambi sisi na wazee wetu;
tumetenda maovu, tumefanya mabaya.
7Wazee wetu walipokuwa Misri,
hawakujali matendo ya ajabu ya Mungu;
hawakukumbuka wingi wa fadhili zake,
bali walimwasi kando ya bahari ya Shamu.
8Hata hivyo Mungu aliwaokoa kama alivyoahidi,
ili aoneshe nguvu yake kuu.
9Aliikemea bahari ya Shamu ikakauka;
akawapitisha humo kama katika nchi kavu.
10Aliwaokoa mikononi mwa waliowachukia;
aliwaokoa kutoka kwa nguvu za maadui zao.
11Maji ya bahari yaliwafunika maadui zao;
wala hakusalia hata mmoja wao.
12Hapo watu wake wakaamini maneno yake,
wakamwimbia tenzi za sifa yake.
13Lakini mara walisahau matendo yake,
wakaacha kutegemea shauri lake.
14Walijawa na tamaa kubwa kule jangwani,
wakamjaribu Mungu kule nyikani.
15Naye akawapa kile walichoomba,
lakini akapeleka maradhi mabaya kati yao.
16
40Hasira ya Mwenyezi-Mungu ikawawakia watu wake,
akachukizwa sana na hao waliokuwa mali yake.
41Akawatia makuchani mwa watu wa mataifa,
hao wenye kuwachukia wakawatawala.
42Maadui zao waliwakandamiza,
wakawatumikisha kwa nguvu.
43Mara nyingi Mungu aliwaokoa watu wake,
lakini wao wakachagua kumwasi,
wakazidi kuzama katika uovu wao.
44Hata hivyo Mungu alizijali taabu zao,
wakati aliposikia kilio chao;
45kwa ajili yao alilikumbuka agano lake,
akawahurumia kwa wingi wa fadhili zake.
46Aliwafanya waliowakandamiza wawaonee huruma.
47Utuokoe, ee Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu,
utukusanye pamoja kutoka kwa mataifa,
tupate kulisifu jina lako takatifu,
na kuona fahari juu ya sifa zako.
48Asifiwe Mwenyezi-Mungu, Mungu wa Israeli,
tangu milele na hata milele!
Na watu wote waseme: “Amina!”
Asifiwe Mwenyezi-Mungu!
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.