Zaburi 75 - Kiswahili Study Bible

Mungu hakimu(Kwa Mwimbishaji: mtindo “Usiharibu”. Zaburi ya Asafu. Wimbo)

1Tunakushukuru, ee Mungu,

tunakushukuru!

Tunatangaza ukuu wa jina lako

na kusimulia juu ya matendo yako makuu.

2Mungu asema: “Mimi nimeweka wakati maalumu!

Wakati huo nitahukumu kwa haki.

3Nchi ikitetemeka na vyote vilivyomo,

mimi ndiye ninayeitegemeza misingi yake.

4Nawaambia wenye kiburi:

‘Acheni kujigamba’;

na waovu: ‘Msioteshe pembe za kiburi!

5Msijione kuwa watu wa maana sana,

wala kusema maneno ya majivuno.’”

6Hukumu haitoki mashariki au magharibi;

wala haitoki nyikani au mlimani.

7Mungu mwenyewe ndiye hakimu;

humshusha mmoja na kumkweza mwingine.

8Mwenyezi-Mungu, anashika kikombe mkononi,

kimejaa divai kali ya hasira yake;

anaimimina na waovu wote wanainywa;

naam, wanainywa mpaka tone la mwisho.

9Lakini mimi nitafurahi milele,

nitamwimbia sifa Mungu wa Yakobo.

10Atavunja nguvu zote za watu waovu;

lakini nguvu za waadilifu ataziimarisha.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help