Zaburi 61 - Kiswahili Study Bible

Kuomba ulinzi(Kwa Mwimbishaji: na ala za nyuzi za muziki. Zaburi ya Daudi)

1Ee Mungu, usikie kilio changu,

usikilize sala yangu.

2Ninakulilia kutoka miisho ya dunia,

nikiwa nimevunjika moyo.

Uniongoze juu kwenye mwamba mkubwa

3maana wewe ndiwe kimbilio langu,

kinga yangu imara dhidi ya adui.

4Naomba nikae nyumbani mwako milele

nipate usalama chini ya mabawa yako.

5Ee Mungu, umezisikia ahadi zangu,

umenijalia sehemu yangu unayowapa wale wakuchao.

6Umjalie mfalme maisha marefu,

miaka yake iwe ya vizazi vingi.

7Atawale milele mbele yako, ee Mungu;

fadhili na uaminifu wako vimlinde.

8Hivyo nitakuimbia nyimbo za sifa,

nikizitekeleza ahadi zangu kila siku.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help