Zaburi 95 - Kiswahili Study Bible

Utenzi wa kumsifu Mungu

1Njoni tumwimbie Mwenyezi-Mungu,

tumshangilie mwamba wa wokovu wetu!

2Twende mbele zake na shukrani;

tumshangilie kwa nyimbo za sifa.

3Maana Mwenyezi-Mungu, ni Mungu mkuu;

yeye ni Mfalme mkuu juu ya miungu yote.

4Vilindi vyote vya dunia vimo mikononi mwake,

vilele vya milima ni vyake.

5Bahari ni yake, ndiye aliyeifanya;

kwa mikono yake aliiumba nchi kavu.

6Njoni tusujudu na kumwabudu;

tumpigie magoti Mwenyezi-Mungu, Muumba wetu!

7Maana yeye ni Mungu wetu,

nasi ni watu wa kundi lake,

ni kondoo wake anaowachunga.

Laiti leo mngesikiliza sauti yake:

8“Msiwe wakaidi kama kule Meriba,

kama walivyokuwa kule Masa jangwani,

9wazee wenu waliponijaribu na kunipima,

ingawa walikuwa wameona mambo niliyowatendea.

10Kwa miaka arubaini nilichukizwa nao,

nikasema: ‘Kweli, hawa ni watu waliopotoka!

Hawajali kabisa njia zangu!’

11Basi, nilikasirika, nikaapa:

‘Hawataingia mahali pangu pa pumziko!’”

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help