Zaburi 12 - Kiswahili Study Bible

Kuomba msaada(Kwa Mwimbishaji: mtindo wa Sheminithi. Zaburi ya Daudi)

1Fanya haraka, ee Mwenyezi-Mungu!

Watu wema wamekwisha;

waaminifu wametoweka miongoni mwa watu.

2Kila mmoja humdanganya mwenzake,

husema kwa kudanganya na kwa moyo wa unafiki.

3Ee Mwenyezi-Mungu

uikomeshe hiyo midomo ya udanganyifu,

na ndimi hizo zinazojigamba kupindukia.

4Wao husema: “Kwa ndimi zetu tutashinda;

midomo tunayo, nani awezaye kututawala?”

5Lakini Mwenyezi-Mungu asema:

“Kwa sababu maskini wanadhulumiwa,

na wahitaji wanapiga kite, sasa naja,

nami nitawapa usalama wanaoutazamia.”

6Neno la Mwenyezi-Mungu ni safi,

safi kama fedha iliyosafishwa katika tanuri,

naam, kama fedha iliyosafishwa mara saba.

7Utulinde, ee Mwenyezi-Mungu,

utukinge daima na kizazi hiki kiovu.

8Waovu wanazunguka kila mahali;

upotovu unatukuzwa kati ya watu.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help