Zaburi 127 - Kiswahili Study Bible

Bila Mungu kazi ya binadamu haifai(Wimbo wa Kwenda Juu, wa Solomoni)

1Mwenyezi-Mungu asipoijenga nyumba,

waijengao wanajisumbua bure.

Mwenyezi-Mungu asipoulinda mji,

waulindao wanakesha bure.

2Mnajisumbua bure kuamka mapema asubuhi

na kuchelewa kwenda kupumzika jioni,

mjipatie chakula kwa jasho lenu.

Mungu huwaruzuku walio wake hata walalapo.

3Watoto ni riziki kutoka kwa Mwenyezi-Mungu;

watoto ni tuzo lake kwetu sisi.

4Watoto waliozaliwa wazazi wakiwa bado vijana,

ni kama mishale mikononi mwa askari.

5Heri mtu aliye na mishale hiyo kwa wingi.

Hatashindwa atakapokabiliana na adui mahakamani.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help