1Toka upeo wa unyonge wangu,
nakulilia, ee Mwenyezi-Mungu.
2Ee Bwana, sikia sauti yangu,
uitegee sikio sauti ya ombi langu.
3Kama, ee Mwenyezi-Mungu ungekumbuka maovu yetu
nani, ee Bwana, angeweza kusalimika?
4Lakini kwako twapata msamaha,
ili sisi tukuheshimu.
5Namtumainia Mwenyezi-Mungu kwa moyo wangu wote;
nina imani sana na neno lake.
6Ninamtumainia Mwenyezi-Mungu
kuliko walinzi wanavyongojea pambazuko;
kuliko walinzi wanavyongojea kuche asubuhi.
7Ee Israeli, umtumainie Mwenyezi-Mungu,
maana kwake Mwenyezi-Mungu kuna fadhili,
kwake kuna nguvu kubwa ya kutukomboa.
8Yeye atawakomboa watu wa Israeli
kutoka katika maovu yao yote.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.