Zaburi 130 - Kiswahili Study Bible

Kuomba msaada(Wimbo wa Kwenda Juu)

1Toka upeo wa unyonge wangu,

nakulilia, ee Mwenyezi-Mungu.

2Ee Bwana, sikia sauti yangu,

uitegee sikio sauti ya ombi langu.

3Kama, ee Mwenyezi-Mungu ungekumbuka maovu yetu

nani, ee Bwana, angeweza kusalimika?

4Lakini kwako twapata msamaha,

ili sisi tukuheshimu.

5Namtumainia Mwenyezi-Mungu kwa moyo wangu wote;

nina imani sana na neno lake.

6Ninamtumainia Mwenyezi-Mungu

kuliko walinzi wanavyongojea pambazuko;

kuliko walinzi wanavyongojea kuche asubuhi.

7Ee Israeli, umtumainie Mwenyezi-Mungu,

maana kwake Mwenyezi-Mungu kuna fadhili,

kwake kuna nguvu kubwa ya kutukomboa.

8Yeye atawakomboa watu wa Israeli

kutoka katika maovu yao yote.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help