1 Watateketezwa kama kichaka cha miiba,
kama vile nyasi zilizokauka.
11Kwako kumetoka aliyepanga maovu dhidi ya Mwenyezi-Mungu
aliyefanya njama za ulaghai.
12Mwenyezi-Mungu awaambia hivi watu wake:
“Ingawa Waashuru ni wengi na wenye nguvu,
wao wataangushwa na kuangamizwa.
Ingawa nimewatesa nyinyi watu wangu,
sitawateseni tena zaidi.
13Sasa nitaivunja nira ya Ashuru shingoni mwenu,
na minyororo waliyowafungia nitaikatakata.”
14Mwenyezi-Mungu ameamuru hivi kuhusu Ninewi:
“Hutapata wazawa kulidumisha jina lako.
Sanamu zako za kuchonga na za kusubu,
nitazivunjavunja nyumbani mwa miungu yako.
Mimi nitakuchimbia kaburi lako,
maana wewe hufai kitu chochote.”
15 Taz Isa 52:7 Enyi watu wa Yuda tazameni:
Anakuja kutoka mlimani mtu anayeleta habari njema,
mjumbe ambaye anatangaza amani.
Adhimisheni sikukuu zenu, enyi watu wa Yuda,
timizeni nadhiri zenu,
maana waovu hawatawavamia tena,
kwani wameangamizwa kabisa.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.