1Hapo Mwenyezi-Mungu alimjibu Yobu kutoka dhoruba:
2“Nani wewe unayevuruga mashauri yangu
kwa maneno yasiyo na akili?
3Jikaze kama mwanamume,
nami nitakuuliza nawe utanijibu.
4“Ulikuwa wapi nilipoiweka misingi ya dunia?
Niambie, kama una maarifa.
5Ni nani aliyeweka vipimo vyake, wajua bila shaka!
Au nani aliyelaza kamba juu yake kuipima?
6Je, nguzo za dunia zimesimikwa juu ya nini,
au nani aliyeliweka jiwe lake la msingi,
7
37Nani mwenye akili ya kuweza kuhesabu mawingu,
au kuinamisha viriba vya maji huko mbinguni?
38ili vumbi duniani igandamane
na udongo ushikamane na kuwa matope?
39“Je, waweza kumwindia simba mawindo yake
au kuishibisha hamu ya wana simba;
40wanapojificha mapangoni mwao,
au kulala mafichoni wakiotea?
41Ni nani awapaye kunguru chakula chao,
makinda yao yanaponililia mimi Mungu,
na kurukaruka huku na huko kwa njaa?
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.