Zaburi 114 - Swahili Common Language DC Bible

Mungu na watu wake

1Watu wa Israeli walipotoka Misri,

wazawa wa Yakobo walipotoka ugenini,

2Yuda ikawa maskani ya Mungu,

Israeli ikawa milki yake.

3Bahari iliona hayo ikakimbia;

mto Yordani ukaacha kutiririka!

4Milima ilirukaruka kama kondoo dume;

vilima vikaruka kama wanakondoo!

5Ee bahari, imekuwaje hata ukakimbia?

Nawe Yordani, kwa nini ukaacha kutiririka?

6Enyi milima, mbona mliruka kama kondoo dume?

Nanyi vilima, mmerukaje kama wanakondoo?

7Tetemeka, ee dunia mbele yake Mwenyezi-Mungu;

tetemeka mbele ya Mungu wa Yakobo,

8anayeugusa mwamba ukawa bwawa la maji,

nayo majabali yakawa chemchemi za maji!

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help