Yobu 4 - Swahili Common Language DC Bible

Hoja ya Elifazi(4:1–14:22)

1Kisha Elifazi yule Mtemani akamjibu Yobu:

2“Je, mtu akijaribu kukuambia neno utakasirika?

Lakini nani awezaye kujizuia kusema?

3Sikiliza! Wewe umewafundisha wengi,

na kuiimarisha mikono ya wanyonge.

4Maneno yako yamewainua waliokufa moyo,

umewaimarisha waliokosa nguvu.

5Lakini sasa yamekupata, nawe ukakosa subira,

yamekugusa, nawe ukafadhaika.

6Je, kumcha Mungu si ndilo tegemeo lako?

Na unyofu wako si ndilo tumaini lako?

7Fikiri sasa: Nani asiye na hatia ambaye amepata kuangamia?

Au, je, waadilifu wamepata kutupwa?

8Nijuavyo mimi, wapandao uovu na ubaya huvuna hayohayo,

9Mungu huwaangamiza hao kwa pumzi yake,

hao huteketezwa kwa pigo la hasira yake.

10Waovu hunguruma kama simba mkali,

lakini meno yao huvunjwa.

11Simba mwenye nguvu hufa kwa kukosa mawindo,

na watoto wa simba jike hutawanywa!

12“Siku moja, niliambiwa neno kwa siri,

sikio langu lilisikia mnongono wake.

13 Mungu?

Mtu aweza kuwa safi mbele ya Muumba wake?

18Hata watumishi wake, Mungu hana imani nao;

na malaika wake huwaona wana kosa;

19sembuse binadamu viumbe vya udongo,

watu ambao chanzo chao ni mavumbi,

ambao waweza kupondwapondwa kama nondo!

20Binadamu kwa masaa machache tu waweza kuangamia;

huangamia milele bila kuacha hata alama yao!

21Iwapo uzi unaoshikilia uhai wao ukikatwa

wao hufa tena bila kuwa na hekima.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help