1Hekima amejenga nyumba yake,
nyumba yenye nguzo saba.
2Amechinja wanyama wa karamu,
divai yake ameitayarisha,
ametandika meza yake.
3Amewatuma watumishi wake wa kike mjini,
waite watu kutoka kwenye vilele vya miinuko:
4“Yeyote aliye mjinga na aje hapa!”
Na yeyote aliye mpumbavu humwambia:
5“Njoo ukale chakula,
na unywe divai niliyotengeneza.
6Achana na ujinga upate kuishi;
fuata njia ya akili.”
7Anayemkosoa mwenye dharau hupata matusi,
amkaripiaye mwovu huishia kwa kuumizwa.
8Usimwonye mwenye dharau maana atakuchukia;
mwonye mwenye hekima naye atakupenda.
9Mfunze mwenye hekima naye atazidi kuwa na hekima;
mfundishe mwadilifu naye atazidi kuelimika.
10
14Hukaa kitako mlangoni mwa nyumba yake,
huweka kiti chake mahali pa juu mjini,
15na kuwaita watu wapitao njiani,
watu wanaokwenda kwenye shughuli zao:
16“Yeyote aliye mjinga na aje hapa!”
Na yeyote aliye mpumbavu humwambia:
17“Maji ya wizi ni matamu sana;
mkate unaoliwa kwa siri ni mzuri sana.”
18Lakini mjinga hajui kwamba humo mna wafu,
wageni wa mwanamke huyo wamo chini Kuzimu.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.