1 langu limekauka kama kigae;
ulimi wangu wanata kinywani mwangu.
Umeniacha kwenye mavumbi ya kifo.
16Genge la waovu limenizunguka;
wananizingira kama kundi la mbwa;
wamenitoboa mikono na miguu.
17Nimebaki mifupa mitupu;
maadui zangu waniangalia na kunisimanga.
18 toka pembe za nyati hao.
Wimbo wa shukrani22 Taz Ebr 2:12 Nitawasimulia ndugu zangu matendo yako;
nitakusifu kati ya kusanyiko lao:
23Enyi mnaomcha Mwenyezi-Mungu, msifuni!
Mtukuzeni enyi wazawa wote wa Yakobo!
Mcheni Mungu enyi wazawa wote wa Israeli!
24Maana yeye hapuuzi au kudharau unyonge wa mnyonge;
wala hajifichi mbali naye,
ila humsikia anapomwomba msaada.
25Kwa sababu yako ninakusifu
katika kusanyiko kubwa la watu;
nitatimiza ahadi zangu mbele yao wakuchao.
26Maskini watakula na kushiba;
wanaomtafuta Mwenyezi-Mungu watamsifu.
Mungu awajalie kuishi milele!
27Ulimwengu wote utakumbuka na kumrudia Mwenyezi-Mungu;
jamaa zote za mataifa zitamwabudu.
28Maana Mwenyezi-Mungu ni mfalme;
yeye anayatawala mataifa.
29Wenye kiburi wote duniani watasujudu mbele yake;
wote ambao hufa watainama mbele yake,
wote ambao hawawezi kudumisha uhai wao.
30Vizazi vijavyo vitamtumikia;
watu watavisimulia habari za Mwenyezi-Mungu,
31watatangaza matendo yake ya wokovu.
Watu wasiozaliwa bado wataambiwa:
“Mwenyezi-Mungu ndiye aliyefanya hayo!”
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.