Zaburi 1 - Swahili Common Language DC Bible

KITABU CHA KWANZA(Zaburi 1–41)Furaha ya kweli

1Heri mtu asiyefuata shauri la waovu,

asiyeshiriki njia za wenye dhambi,

wala kujumuika na wenye dharau;

2bali huifurahia sheria ya Mwenyezi-Mungu,

na kuitafakari mchana na usiku.

3Huyo ni kama mti uliopandwa kando ya vijito,

unaozaa matunda kwa wakati wake,

na majani yake hayanyauki.

Kila afanyalo hufanikiwa.

4Lakini waovu sivyo walivyo;

wao ni kama makapi yapeperushwayo na upepo.

5Kwa hiyo watu waovu wataanguka wakati wa hukumu,

wenye dhambi hawatakaa na kusanyiko la waadilifu.

6Maana Mwenyezi-Mungu huziongoza njia za waadilifu;

lakini njia za waovu zitaishia katika maangamizi.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help