Zaburi 94 - Swahili Common Language DC Bible

Mungu hakimu wa wote

1Ee Mwenyezi-Mungu, Mungu mwenye kulipiza kisasi,

ewe Mungu mlipiza kisasi, ujitokeze!

2Usimame, ee hakimu wa watu wote;

uwaadhibu wenye kiburi wanavyostahili!

3Waovu wataona fahari hata lini?

Watajisifia mpaka lini, ee Mwenyezi-Mungu?

4Hata lini waovu watajigamba kwa maneno?

Waovu wote watajivuna mpaka lini?

5Wanawaangamiza watu wako, ee Mwenyezi-Mungu,

wanawakandamiza hao walio mali yako.

6Wanawaua wajane na wageni;

wanawachinja yatima!

7Wanasema: “Mwenyezi-Mungu haoni,

Mungu wa Yakobo hajui!”

8Enyi wajinga wa mwisho, fikirini kidogo!

Enyi wapumbavu, mtapata lini maarifa?

9Aliyefanya sikio, je, hawezi kusikia?

Aliyeumba jicho, je, hawezi kuona?

10Mwenye kutawala mataifa, je, hawezi kuadhibu?

Mkufunzi wa wanadamu, je, hana maarifa?

11

18Nilipohisi kwamba ninateleza,

fadhili zako, ee Mwenyezi-Mungu, zilinitegemeza.

19Mahangaiko ya moyo wangu yanapozidi,

wewe wanifariji na kunifurahisha.

20Wewe huwezi kushirikiana na mahakimu dhalimu,

wanaotunga kanuni za kutetea maovu.

21Wao wanaafikiana kuwaangamiza waadilifu,

na kuwahukumu watu wasio na hatia wauawe.

22Lakini Mwenyezi-Mungu ni ngome yangu;

Mungu wangu ni mwamba wa usalama wangu.

23Uovu wao atawarudishia wao wenyewe,

atawafutilia mbali kwa sababu ya ubaya wao.

Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu, atawafutilia mbali!

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help