Isaya 49 - Swahili Common Language DC Bible

Israeli: Mwanga wa mataifa

1

7Mwenyezi-Mungu, Mkombozi na Mtakatifu wa Israeli,

amwambia hivi yule anayedharauliwa mno,

yule anayechukiwa na mataifa,

na ambaye ni mtumishi wa watawala:

“Wafalme watakuona nao watasimama kwa heshima,

naam, wakuu watainama na kukusujudia

kwa sababu yangu mimi Mwenyezi-Mungu

ambaye hutimiza ahadi zangu;

kwa sababu yangu mimi Mtakatifu wa Israeli

ambaye nimekuteua wewe.”

Kujengwa upya kwa Yerusalemu

8

13Imbeni kwa furaha, enyi mbingu!

Shangilia ewe dunia.

Pazeni sauti mwimbe enyi milima,

maana Mwenyezi-Mungu amewafariji watu wake,

naam, atawaonea huruma watu wake wanaoteseka.

14Wewe Siyoni wasema:

“Mwenyezi-Mungu ameniacha;

hakika Bwana wangu amenisahau.”

15Lakini Mwenyezi-Mungu asema:

“Je, mama aweza kumsahau mwanawe anayenyonya,

asimwonee huruma mtoto wa tumbo lake?

Hata kama mama aweza kumsahau mwanawe,

mimi kamwe sitakusahau.

16Nimekuchora katika viganja vyangu;

kuta zako naziona daima mbele yangu.

17Watakaokujenga upya wanakuja haraka,

wale waliokuharibu wanaondoka.

18Inua macho uangalie pande zote;

watu wako wote wanakusanyika na kukujia.

Naapa kwa nafsi yangu mimi Mwenyezi-Mungu,

watu wako watakuwa kwako kama mapambo,

utawafurahia kama afanyavyo bibi arusi na utaji wake.

19“Kweli umekumbana na uharibifu,

makao yako yamekuwa matupu,

na nchi yako imeteketezwa.

Lakini sasa itakuwa ndogo mno kwa wakazi wake;

na wale waliokumaliza watakuwa mbali.

20Wanao waliozaliwa uhamishoni,

watakulalamikia wakisema:

‘Nchi hii ni ndogo mno;

tupatie nafasi zaidi ya kuishi.’

21Hapo ndipo utakapojiuliza mwenyewe:

‘Nani aliyenizalia watoto wote hawa?

Nilifiwa na wanangu bila kupata wengine.

Nilipelekwa uhamishoni na kutupwa mbali;

nani basi aliyewalea watoto hawa?

Mimi niliachwa peke yangu,

sasa, hawa wametoka wapi?’”

22Bwana Mungu asema hivi:

“Nitayapungia mkono mataifa;

naam, nitayapa ishara,

nayo yatawabeba watoto wenu wa kiume,

kadhalika na watoto wenu wa kike

na kuwarudisha kwako.

23Wafalme watakushughulikia,

na malkia watakutengenezea chakula.

Watakusujudia na kukupa heshima,

na kuramba vumbi iliyo miguuni pako.

Hapo utatambua kuwa mimi ni Mwenyezi-Mungu;

wote wanaonitegemea hawataaibika.”

24Watu wa Yerusalemu walalamika:

“Je, shujaa aweza kunyanganywa nyara zake?

Au mateka wa mtu katili waweza kuokolewa?”

25Mwenyezi-Mungu ajibu:

“Naam! Hata nyara za shujaa zitachukuliwa,

mateka wa mtu katili wataokolewa.

Mimi mwenyewe nitawakabili maadui zako,

mimi mwenyewe nitawaokoa watoto wako.

26Nitawafanya wanaokukandamiza watafunane;

watalewa damu yao wenyewe kama divai.

Hapo binadamu wote watatambua kwamba

mimi ni Mwenyezi-Mungu, Mwokozi wako,

mimi ni Mkombozi wako, Mwenye Nguvu wa Yakobo.”

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help