Zaburi 150 - Swahili Common Language DC Bible

Zaburi ya kumsifu Mungu

1Msifuni Mwenyezi-Mungu!

Msifuni Mungu katika patakatifu pake;

msifuni katika mbingu zake kuu.

2Msifuni kwa sababu ya matendo yake makuu;

msifuni kwa ajili ya utukufu wake mkuu.

3Msifuni kwa mlio wa tarumbeta;

msifuni kwa zeze na kinubi!

4Msifuni kwa ngoma na kucheza;

msifuni kwa filimbi na banjo!

5Msifuni kwa kupiga matoazi.

Msifuni kwa matoazi ya sauti kubwa.

6Kila kiumbe hai kimsifu Mwenyezi-Mungu!

Msifuni Mwenyezi-Mungu!

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help