Zaburi 48 - Swahili Common Language DC Bible

Siyoni mji wa Mungu(Kwa Mwimbishaji. Zaburi ya Wakorahi)

1Mwenyezi-Mungu, ni mkuu; astahili kusifiwa sana

katika mji wake na mlima wake mtakatifu.

2 Taz Mat 5:35 Mlima Siyoni huko kaskazini, wapendeza kwa urefu;

mji wa Mfalme mkuu ni furaha ya ulimwengu.

3Mungu anazilinda ngome zake;

yeye amejionesha kuwa ngome ya usalama.

4Wafalme walikusanyika,

wakaenda pamoja kushambulia.

5Lakini walipouona mji wa Siyoni, wakashangaa;

wakashikwa na hofu, wakatimua mbio.

6Hofu kuu iliwashika,

wakasikia uchungu kama mama anayejifungua,

7kama waliokumbwa na kimbunga cha mashariki

ambacho huzivunjavunja meli za Tarshishi.

8Yote tuliyosikia tumejionea wenyewe

katika mji wa Mwenyezi-Mungu wa majeshi,

naam, katika mji wa Mungu wetu;

Mungu atauimarisha milele.

9Ee Mungu, twazitafakari fadhili zako,

tukiwa hekaluni mwako.

10Jina lako lasifika kila mahali,

sifa zako zaenea popote duniani.

Kwa mkono wako umetenda kwa haki;

11watu wa Siyoni na wafurahi!

Watu wa Yuda na washangilie,

kwa sababu ya maamuzi yako ya haki!

12Tembeeni huko Siyoni mkauzunguke,

mkaihesabu minara yake.

13Zitazameni kuta zake

na kuchunguza ngome zake;

mpate kuvisimulia vizazi vijavyo, kwamba:

14“Huyu ni Mungu, Mungu wetu milele!

Atakuwa kiongozi wetu milele!”

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help