Zaburi 112 - Swahili Common Language DC Bible

Furaha ya mtu mwema

1Msifuni Mwenyezi-Mungu!

Heri mtu anayemcha Mwenyezi-Mungu,

anayefurahia sana kutii amri zake.

2Wazawa wake watakuwa wenye nguvu nchini;

watoto wa wanyofu watapata baraka.

3Nyumbani kwake kutakuwa na mali nyingi;

uadilifu wake wadumu milele.

4Mtu mwema huangaziwa mwanga gizani;

mtu mwenye huruma, mpole na mwadilifu.

5Mtu mkarimu akopeshaye bila faida, hufanikiwa;

mtu afanyaye shughuli zake kwa kutumia haki.

6Mwadilifu hatashindwa kamwe,

huyo atakumbukwa milele.

7Hana haja ya kuogopa akipata habari mbaya;

ana moyo thabiti na humtegemea Mwenyezi-Mungu.

8Yuko imara moyoni, wala hataogopa;

naye atawaona maadui zake wanashindwa.

9 Taz 2 Kor 9:9 Hutoa kwa ukarimu, huwapa maskini;

uadilifu wake wadumu milele.

Nguvu yake inatukuzwa kwa heshima.

10Watu waovu huona hayo na kuudhika;

husaga meno kwa chuki na kutoweka,

matazamio ya mtu mbaya huishia patupu.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help