Zaburi 11 - Swahili Common Language DC Bible

Kumtumainia Mungu(Kwa Mwimbishaji. Zaburi ya Daudi)

1Kwake Mwenyezi-Mungu nakimbilia usalama;

mnawezaje basi kuniambia:

“Ruka kama ndege, mpaka milimani,

2maana waovu wanavuta pinde;

wameweka mishale tayari juu ya uta,

wawapige mshale watu wema gizani!

3Kama misingi ikiharibiwa,

mtu mwadilifu atafanya nini?”

4Mwenyezi-Mungu yumo katika hekalu lake takatifu;

kiti cha enzi cha Mwenyezi-Mungu kiko mbinguni.

Kwa macho yake huwachungulia wanadamu,

na kujua kila kitu wanachofanya.

5Mwenyezi-Mungu huwapima waadilifu na waovu;

huwachukia kabisa watu wakatili.

6Atawanyeshea waovu makaa ya moto na madini ya kiberiti;

upepo wa hari utakuwa ndio adhabu yao.

7Mwenyezi-Mungu ni mwadilifu na apenda uadilifu;

watu wanyofu watakaa pamoja naye.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help